Makala Mbalimbali

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Rais Samia Aongoza Taifa Kumuaga Hayati Jenista Joakim Mhagama

Dodoma, 13 Desemba 2025 Taifa limeingia katika majonzi makubwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama. Kufuatia tukio tukio hilo lililogusa hisia za wengi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo ameongoza familia, viongozi wa kitaifa, wabunge pamoja na waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu iliyofanyika katika Kanisa la Mwenyeheri Maria-Theresa Ledochowska, Parokia ya Kiwanja cha Ndege, Jimbo Kuu Katoliki Dodoma.

RAIS SAMIA ATOA MSIMAMO MKALI KUHUSU VURUGU ZA OKTOBA 29 NA MUSTAKABALI WA TAIFA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,amezungumza na Wazee wa Jiji la Dar es Salaam na taifa kwa ujumla, akifafanua kwa kina kuhusu matukio ya Oktoba 29, 2025, athari zake, chanzo chake na mwelekeo wa serikali katika kulinda amani na umoja wa nchi.

RAIS SAMIA AZINDUA TUME HURU YA UCHUNGUZI WA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI YA UCHAGUZI MKUU 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025. Tume hiyo ameiunda tarehe 18 Novemba 2025 kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi ya mwaka 2023 (Sura ya 32), na amemkabidhi uenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mohamed Chande Othman, huku akiwa ameipa muda wa miezi mitatu kutekeleza majukumu yake.

RAIS SAMIA AANZA MKAKATI MPYA: MIRADI KUTEKELEZWA KWA FEDHA ZA NDANI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweka wazi dira mpya ya Serikali ya Awamu ya Sita wakati akiwaapisha Mawaziri na Manaibu Mawaziri 56 jijini Dodoma, ambapo ameeleza dhamira yake ya kuharakisha maendeleo kwa kutekeleza miradi kwa kutumia rasilimali za ndani na kuimarisha uwajibikaji wa viongozi wake.

RAIS SAMIA AZINDUA BUNGE LA 13 AKITOA WITO WA AMANI, MAELEWANO NA MAENDELEO YA TAIFA

Dodoma, Novemba 14, 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, siku ya leo amezindua Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutoa wito wa umoja, maelewano na amani nchini, huku akiongoza Wabunge pamoja na wageni waalikwa kusimama kwa heshima na kuwakumbuka wananchi waliopoteza maisha katika vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025, katika miji ya Arusha, Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza na Songwe.

HOTUBA YA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN WAKATI WA KUAPISHWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, TAREHE 3 NOVEMBA, 2025 - CHAMWINO, DODOMA

Nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuturuzuku uhai na kutuwezesha kushiriki sherehe hizi za kihistoria kwa Taifa letu. Pili niwashukuru Watanzania wote kwa imani yao kwa Chama cha Mapinduzi, na kwa mapenzi makubwa, na kutupa mimi na Makamu wa Rais fursa hii adhimu ya kuwatumikia.

DKT SAMIA AWEKA WAZI AJENDA KUU TATU ZA CCM KATIKA MIAKA MITANO IJAYO.

Mgombea wa urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameeleza kuwa ajenda kuu tatu za chama hicho katika kuongoza taifa ni kuliheshimisha taifa la Tanzania ndani na nje ya nchi, kukuza maendeleo ya kiuchumi, na kuboresha huduma za kijamii kwa Watanzania wote.

RAIS DK. SAMIA SULUHU HASSAN ATAJA NEEMA MPYA KWA WANA TABORA

Mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea na ziara yake ya kampeni mkoani Tabora, ambako ameahidi miradi mikubwa ya maendeleo inayogusa moja kwa moja maisha ya wananchi.

KIPAUMBELE CHETU NI AMANI, KABLA NA BAADA YA UCHAGUZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa watanzania wote kulinda amani ya taifa hasa kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

RAIS DK. SAMIA AZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA NA SAFARI ZA MIZIGO ZA SGR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameandika historia mpya ya mageuzi ya kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji, hii ni baada ya kuzindua rasmi Bandari Kavu ya Kwala iliyopo Mkoani Pwani, pamoja na kuzindua rasmi kwa safari za mizigo kwa kutumia Reli ya Kisasa (SGR), ifikapo Agosti 4, 2025.

RAIS SAMIA AZINDUA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameandika ukurasa mpya katika historia ya maendeleo ya taifa kwa kuzindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

RAIS DK. SAMIA SULUHU HASSAN ATAKA UWEKEZAJI ZAIDI NA USIMAMIZI WA KILIMO NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza Wakuu wa Mikoa kote nchini kusimamia ipasavyo sekta ya kilimo kwa kuhakikisha inakuwa kipaumbele katika maeneo yao, ikiwa ni hatua ya kuimarisha uzalishaji na mchango wa kilimo katika uchumi wa taifa.

HOTUBA YA KIHISTORIA YA RAIS DK. SAMIA SULUHU HASSAN KULIHUTUBIA BUNGE LA 12 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Katika kilele cha kufunga pazia la Bunge la 12, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa hotuba ya kihistoria iliyochukua takribani saa mbili na nusu, akitoa mwelekeo wa taifa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu pamoja na taarifa ya utekelezaji wa ahadi na miradi ya maendeleo kwa miaka minne toka alipoingia madarakani.

MRADI WA MAJI WA SHILINGI BILIONI 12.8 WAZINDULIWA LAMADI – SIMIYU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi mradi mkubwa wa maji katika kata ya Lamadi, Wilaya ya Busega, mkoani Simiyu. Mradi huo umegharimu shilingi bilioni 12.8 na unalenga kuhudumia zaidi ya wananchi 85,000 kutoka vijiji vya Lamadi, Lutubiga na Mkula.

RAIS SAMIA AZINDUA DARAJA LA J.P. MAGUFULI – KIGONGO–BUSISI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo–Busisi) ambalo ni sehemu ya miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita.

RAIS SAMIA: ELIMU YA UFUNDI NI MLANGO WA AJIRA KWA VIJANA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imeamua kuipa msukumo mkubwa elimu ya amali na ufundi ili kuwawezesha vijana kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri au kuajiriwa moja kwa moja baada ya kuhitimu sekondari.

RAIS DKT. SAMIA ASHIRIKI SHEREHE YA KUFUNGA KOZI YA MAAFISA NA WAKAGUZI WASAIDIZI WA JESHI LA POLISI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 9 Juni 2025, ameshiriki sherehe ya kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi katika viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Polisi, Kurasini, Jijini Dar es Salaam.

RAIS SAMIA ACHANGIA MILIONI 100 KUSAIDIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU BAGAMOYO.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amelisifu Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa kuonesha mfano bora wa utumishi wa dini unaogusa maisha ya watu kwa vitendo.

RAIS SAMIA ASIFU MAGEUZI YA MASHIRIKA NA TAASISI ZA UMMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameeleza kuridhishwa kwake na maendeleo yanayoshuhudiwa katika mashirika na taasisi za umma, ambapo serikali imepokea gawio na michango yenye thamani ya Shilingi trilioni 1.28.

MHE RAIS DKT, SAMIA AZINDUA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2025–2030

Dodoma, Tanzania – Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha 2025 hadi 2030,

Tanzania Yazindua Rasmi Sera Mpya ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2024

Katika hatua ya kihistoria inayolenga kuimarisha ushawishi wa Tanzania katika medani ya kimataifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2024, tarehe 19 Mei 2024 jijini Dar es salaam.

or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook