Rais Samia Aongoza Taifa Kumuaga Hayati Jenista Joakim Mhagama
Dec 2025Dodoma, 13 Desemba 2025 Taifa limeingia katika majonzi makubwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama. Kufuatia tukio tukio hilo lililogusa hisia za wengi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo ameongoza familia, viongozi wa kitaifa, wabunge pamoja na waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu iliyofanyika katika Kanisa la Mwenyeheri Maria-Theresa Ledochowska, Parokia ya Kiwanja cha Ndege, Jimbo Kuu Katoliki Dodoma.





