Reconciliation (Maridhiano)

Kujenga jamii inayofurahia haki sawa mbele ya sheria, bila ubaguzi na ambayo hutoa fursa sawa za kiuchumi kwa wote.

Resilience (Ustahimilivu)

Katika safari iliyo mbele, Tanzania itakumbwa na misukosuko. Iwe ni kiuchumi, kimazingira, kijamii au kisiasa lakini lazima tujenge ustahimilivu.

Reforms (Mageuzi)

Serikali itajitahidi kufanya mabadiliko katika mfumo wa kisiasa, kiuchumi na uchaguzi wa Tanzania.

Rebuild (Ujenzi mpya)

Lengo kuu linapaswa kuwa kukuza uchumi wa Tanzania. Uchumi utakaosaidia kuongeza ajira kwa vijana na kufungua fursa kwa makundi yote ya kijamii nchini

Taarifa Muhimu

RAIS DK. SAMIA AZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA NA SAFARI ZA MIZIGO ZA SGR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameandika historia mpya ya mageuzi ya kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji, hii ni baada ya kuzindua rasmi Bandari Kavu ya Kwala iliyopo Mkoani Pwani, pamoja na kuzindua rasmi kwa safari za mizigo kwa kutumia Reli ya Kisasa (SGR), ifikapo Agosti 4, 2025.

RAIS SAMIA AZINDUA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameandika ukurasa mpya katika historia ya maendeleo ya taifa kwa kuzindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kuijenga Tanzania yenye uchumi imara, jamii jumuishi na ustawi kwa wote. Uzinduzi huo umefanyika jijini Dodoma, ambapo Rais Samia amebainisha kuwa utekelezaji wa dira hiyo utaanza rasmi Julai 1, 2026, mara baada ya kukamilika kwa Dira ya Maendeleo 2025.

Soma Zaidi

Makala Mbalimbali

Soma Zaidi

Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ainua uchumi na huduma za afya wilaya ya Temeke

Katika ziara ya Dira ya Samia kwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Sixtus Mapunda alitoa maelezo ya kina kuhusu juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha uchumi na huduma za afya za Wilaya ya Temeke.

Soma Zaidi

Tamasha la Kizimkazi Lapandishwa Hadhi Rasmi:

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza kuwa Tamasha la Kizimkazi la kila mwaka liingizwe rasmi kwenye orodha ya matukio yanayochangia kukuza utalii nchini Tanzania.

Matunda ya ziara ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan Mkoani Morogoro.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameanza rasmi ziara ya siku sita mkoani Morogoro.

Uzinduzi wa Treni ya SGR Unakuja na Mapinduzi Makubwa Nchini

Leo, watanzania tunajivunja kuzindua rasmi sehemu ya kwanza ya reli ya kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan

Uzinduzi wa Treni ya Umeme ya SGR Kati ya Dar es Salaam na Dodoma: Mapinduzi ya Usafiri Tanzania

Huduma za treni ya umeme ya Reli ya Kisasa (SGR) kati ya Dar es Salaam na Dodoma imeanzishwa rasmi siku ya Alhamisi, ikitarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya usafiri nchini Tanzania.

or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook